Tuesday, November 29, 2011

3) KANISA LA PERGAMO(Ufunuo 2:12-17)

12)Na kwa malaika lililoko Pergamo andika;
       Haya ndiyo ananenayo yeye aliye na huo upanga mkali, wenye makali kuwili. Napajua ukaapo, ndipo penye kiti cha enzi cha Shetani; nawe walishika sana jina langu, walahukuikana imani yangu, hata katika siku za Antipa shahidi wangu, mwaminifu wangu, aliyeuwawa kati yenu, hapo akaapo Shetani (14) Lakini ndiyo maneno machache washikao mafundisho ya Balaanu, yeye aliyemfundisha Balaki atie ukwazo mbele ya Waisraeli, kwamba wavile vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na kuzini. (15)Vivyo hivyo wewe nawe unao watu wayashikao mafundisho ya Wanikolai vilevile (16) Basi tubu; na usipotubu, naja kwako upesi, nami nitafanya vita juu yao kwa huo upaga wa kinywa changu. (17) Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea


Kanisa la Pergamo
  • Neno Pergamo humaanisha 'Kimo au Mwinuko'
  • Mji wao wa kwanza ulijengwa juu ya kilima chenye mawe mengi kilichoinuka futi elfu moja
  • Kanisa hili lilidumu kati ya miaka ya 313 B.K-538B.K
  • Hapa ni kwamba mateso yote yalikoma
  • Hapa ndipo mfalme Constantine (Konstantino) mwenyewe alijifanya Mkristo, kumbe kanisa lilikuwa katika hatari kubwa ! Kumbe ile ''Siri ya Uasi'' ilipoanzia. Yeye ndiye aliyebadilisha wakati, saa na majira.(alitimiza unabii wa Danieli 7:25)
Sanamu la Constatine
  • Kiti cha enzi cha Shetani humaanisha- mahali anapofanyia kazi, ndipo alipofanya kazi kubwa kwa kutumia Conctatine na kuleta anguko kubwa mpaka leo.

  • Historia haitufahamishi mtu yeyote aliyeitwa 'Antipa', lakini inaelekeza ni kikundi cha watu waliopoteza maisha yao kwa sababu ya upapa(papacy), 'Anti' humaanisha kupinga na 'pa' maana yake ni baba au Papa(pope)

  • Wengine walikana imani yao ili kufainika na utajiri na heshima za kibinadamu au ulimwengu kama vile Baalamu alivyokuwa tayari kuwalaani na kupewa tuzo la thamani (Hesabu 22-25)

  • Biblia ilifika hadi Ikulu za wafalme nao wakaitafsiri vibaya.

  • 2) KANISA LA SMIRNA(Ufunuo 2:8-11)

    (8) Na kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika;
           Haya ndiyo annenayo yeye aliye wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa, kisha akawa hai. (9) Naijua dhiki yako na umaski wako,(lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi bali ni sinagogi la Shetani. (10) Usiogope mambo yatakayokupata; tazama huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa, taji ya uzima. (11) Yeye aliye na sikio, na asikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili

    KANISA LA SMIRNA
    • Neno Smirna humaanisha kitu kinachoonukia vizuri
    • Kanisa hili lilikuwepo kati ya muda au miaka wa mateso na maumivi ambacho kilikuwa miaka ya 100 B.K mpaka 313 B.K
    Mungu hafurahii kuona watu wake wakiteswa, lakini uaminifu na utii wao katika majaribu ulimfurahisha na kuliinua jina la Mwokozi aliyewafia

    Mungu anawaambia kanisa la Smirna kwamba anawajua wale wanaosema kwamba wenyewe ni Wayahudi lakini si Wayahudi, Basi hao Wayahudi ni nani?

    Wayahudi ni wale watu ambao walipewa kwa sana neno la Mungu na kulikataa, ndipo Mungu akaamua kuwapa mataifa katika mwaka wa 33B.K(hili nalo ni somo)

    Lakini kadhalika kulikuwa na Wayahudi fulani ambao walikuwa wanashika neno la Mungu, lakini mtume Paulo anasemaje kuhusu kuwa myahudi kwa uhakikia (Warumi 2:28,29) unasema 'uyahudi wa mtu hauonekani kwa nje bali kwa ndani ambaye sifa yake haitoki kwa mwanadamu bali hutoka kwa Mungu'

    Basi katika wakati ule watu walijidai kumfuata Kristo, lakini katika mioyo yao wakipenda ulimwengu na ubunafsi, lakini kwa wao walilishika neno la Mungu walitaabishwa na kuanza kufuata nyao, desturi na Imani ya Kristo

    SANAMU LA MFALME DIOCLETIAN
    Sasa, maana ya siku kumi ni nini?
    Ni siku za mateso, ni kipindi katika muda wa unabii, siku moja husimama badala ya mwaka mmoja(Tazama Hesabu 14:34; Ezekiel 4:6)
        Kilikuwa ni kipindi ambacho kilikuwepo ndani ya wakati wa kanisa la Smirna (100 B.K-313B.K) ambapo, utawala wa mfalme huyu katili ambaye alikuwa anawatesa watu wa Mungu Utawala wa Mfalme Diocletian, (ambaye anafananishwa na sinagogi la shetani)

    Lakini kumbuka wale watu waliokufa katika Imani hawana cha kuogopa ndio maana Yohana anawatia moyo.



                                                                                                   
                                                                                                               

    Monday, November 28, 2011

    MAKANISA SABA

    1)     KANISA LA EFESO (Ufunuo:2:2-7)


    2)Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume na sio, ukawaona waongo; (3) tena ulikuwa na subira haukuvumilia kwa ajili ya jina langu, wala hukuchoka (4)lakini nina neno juu yako,  ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza (5)basi, kumbukuka ni wapi ulipoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza,  Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu (6) Lakini  unalo neon hili, kwamba wachukia matendo ya wanikolai, ambayo na mimi nayachukia. (7) Yeye aliye na sikio,  na asikie, neon hili ambalo roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa kula matunda ya mti wa uzima, uliyo katika bustani ya Mungu. 




    ·       Efeso humaanisha tamanio


    ·       Kanisa la Efeso lilikuwa ni taa ing’aayo katika giza tororo,lilikuwa likifaulu kila sehemu na watu wenye tamaa,viburi walibadilika.


    ·       Lakini kidogo kidogo badadiliko yalianza kuingia na wengi walipoteza imani yao ile ya kwanza, Je ni nani aliyewapoteza?


    ·       Katika mstari wa sita ,Mungu anasema anawachukia wanikolai, Basi wanikolai ni akina nani?


    ·       Katika Matendo6:5 tunaona kuna mashemasi saba walichaguliwa kuwahudumia wajane kwani walikuwa wanasahulika ndimo kulikuwa na Stefano, Filipo vilevile palikuwepo na Nikolao, pakawa na kikundi cha wanikolao ambao walihubiri habari potofu za Mungu.


    ·       Basi Yohana akaongozwa na roho mtakatifu kuliandikia kanisa la Efeso akiwapa maonyo kutowasikiliza hao,
    • Lakini walipewa chaguo,“yeye aliye na sikio, na asikie neon hili ambalo roho anayaambia makanisa.Yeye ashinaye nitampa kula matunda ya mti wa uzima,ulio katika bustani ya Mungu”